Watu watano wa familia moja wauawa katika kile serikali inasema ni mzozo wa ardhi Mlima Elgon
23rd October, 2015
Siku mbili pekee baada ya kamishna wa kaunti ya Bungoma Maalim Mohammed kutangaza kuwa huenda serikali ikaanzisha operesheni mpya ya kijeshi kukabiliana na wanamgambo wa kundi la Sabaot Land Defense Force {SLDF} wilayani Mlima Elgon, maafa yametokea usiku wa kuamkia leo. Hii ni baada ya watu watano wa familia moja kuuawa katika kile ambacho serikali imesema ni mzozo wa ardhi.