Mzee Mwangi Waichigo ana nywele ndefu ambazo hajazinyoa kwa zaidi ya miaka hamsini
21st October, 2015
Mzee Mwangi Waichigo ana nywele ndefu zinazowasisimua wengi kwa kuwa hajazinyoa kwa zaidi ya miaka hamsini. Anajitambulisha kama mpiganiaji wa Uhuru na japo hakupigania msituni, alikamatwa na wabeberu na kuzuiliwa katika kambi mbalimbali. Anachotaka mzee Daudi kama anavyojulikana na wengi huko nyumbani kwake Kieni mashariki ni kwa vizazi vijavyo kufahamu juhudi za wapiganiaji wa Uhuru za kuliokomboa taifa la Kenya.