Uhuru Kenyatta akariri kuwa maombi ya William Ruto na Joshua Sang itaendelea
21st October, 2015
Kwa mara nyengine siasa za mahakama ya ICC zimejitokeza baada ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kukariri kuwa mikutano ya maombi inayoandaliwa na mrengo wa Jubilee kwa niaba ya naibu wa rais William Ruto na mwanahabari Joshua Sang itaendelea. Kama ilivyopangwa. Matamshi haya yametolewa siku chache tu baada ya jaji wa mahakama ya ICC Chile Osuji kuwaonya viongozi wa Kenya kukoma kutumia hafla za maombi katika kuisuta mahakama hiyo.