Waziri James Macharia awataka wabunge kupitisha mswada wa sheria za afya ili kuepuka utepetevu
16th October, 2015
Waziri wa afya James Macharia amewataka wabunge kuharakisha kupitishwa kwa mswada wa sheria za afya ili kuepuka visa vya utepetevu katika hospitali za umma na za binafsi. Akizungumza katika hafla ya ushirikiano kati ya Uchina na Kenya ili kuboresha sekta ya afya nchini Kenya , Macharia amesema kuwa ni kinyume cha sheria kwa mkenya yeyote kunyimwa matibabu ya dharura kwa sababu ya kukosa pesa