Mvua kubwa inatarajiwa kunyesha katika kaunti ya Mombasa na sehemu kadhaa za Pwani
6th October, 2015
Mvua kubwa inatarajiwa kunyesha katika kaunti ya Mombasa na sehemu kadhaa za Pwani kuanzia usiku wa leo. Haya ni kwa mujibu wa idara ya utabiri wa hali ya anga. Watabiri wamesema huenda mvua hiyo ya zaidi ya milimita thelathini kwa siku tatu mfululizo ikasababisha mafuriko au maporomoko ya ardhi. Idara hiyo sasa imewataka wapwani na wakazi wengine walio sehemu za Mombasa au kaskazini mwa Mombasa, mfano na Mtwapa, kuepuka mikondo ya maji wakati wa mafuriko ili kuepuka hatari.