Seneta wa Machakos Johnstone Muthama apinga madai ya kutoa matamshi ya uchochezi
30th September, 2015
Seneta wa Machakos Johnstone Muthama ameyapinga madai ya kutoa matamshi ya uchochezi na kusema kwamba aliyeyawasilisha malalamishi hayo hakuutathmini vilivyo usemi wake. Hii ni kwa mujibu wa tarifa kwa wanahabari iliyosomwa na seneta wa Bungoma Moses Wetangula aliyeandamana na Muthama. Hata hivyo N.C.I.C imesema kwamba haitegemei malalamishi kutoka kwa mtu binafsi ili kutekeleza majumu yake.