Timu ya raga Impala Saracens na Top Fry Nakuru kupata ujuzi wa mchezo wa raga nchini uingereza
28th September, 2015
Timu ya raga ya wachezaji wasiozidi umri miaka 13 na vile vile timu ya Top Fry Nakuru zitakuwa kati ya timu nyingi kutoka kote nchini ambazo zitapata nafasi ya kupata ujuzi wa mchezo wa raga nchini uingereza. Timu ya Impala itawakilishswa na wachezaji kumi ambao watapata nafasi ya kuzuru nchi za uingereza na vile vile kupata mafunzo ya mchezo wa raga huku pia wakitarajiwa kutazama mechi za kombe la dunia la raga nchini uingereza. Timu ya Impala itapata Udhamin kutoka kwa benki ya Standard Charterd ambao watasimamia gharama ya safari hiyo. timu kutoka Uganda, Botswana, Colombia, Hong Kong, India, Afrika Kusini, Swaziland na Uganda zitashiriki ziara hii nchini uingereza.