Mashine ya Radiotherapy yapata hitilafu katika Hospitali Kuu Ya Kenyatta
3rd September, 2015
Maelfu ya wagonjwa wa maradhi ya saratani wameathirika baada ya mashine moja inayotoa huduma ya Radiotherapy katika Hospitali Kuu ya Kenyatta kuwa na hitilafu. Kulingana na wasimamizi wa hospitali ya Kenyatta uharibifu huo umetokana na matumizi ya kupita kiasi ya huduma hiyo. Haijabainika ni lini mashine hiyo itaanza kufanya kazi upya huku wagonjwa wengi wanaoitegemea huduma hii wasijue la kufanya. Saida Swaleh alizuru hospitali kuu ya Kenyatta na kutuandalia taarifa ifuatayo.