Naibu Rais William Ruto atimua mbio kuwalaki wanariadha wa Kenya waliowasili nchini kutoka Uchina
1st September, 2015
Naibu Rais William Ruto leo amewaacha wengi wakiangua kicheko katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, alipotimua mbio kuwalaki wanariadha wa kenya waliowasili nchini kutoka Uchina.walinzi wa naibu rais walibaki wakidondokwa kijasho wakijaribu kumfikia naibu rais. Mabingwa hao waliinua hadhi ya Kenya kwa kulifanya taifa bora kwenye kinyang’anyiro cha IAAF. Mwanaspoti wetu Lynne Wachira anaarifu.