Isaiah Kiplagat atangaza kurejea kwake kwenye Shirikisho la Riadha nchini
1st September, 2015
Mwenyekiti wa shirikisho la riadha nchini, Isaiah Kiplagat ametangaza kurejea kwake kwenye shirikisho la riadha nchini baada ya likizo ya muda wa miezi mitatu. Kiplagat alikosa kufaulu katika azma yake ya kuchaguliwa kama naibu mwenyekiti wa shirikisho la riadha nchini, IAAF. Hata hivyo, alisisitiza kuwa kurejea kwake ni mwanzo wa matayarisho ya kustaafu kwake kutoka riadha.