Mbwa 1,500 wachanjwa Laikipia kwenye kampeini ya kupunguza ugonjwa wa kichaa cha mbwa
18th August, 2015
Ugonjwa wa kichaa cha mbwa huwaua watu 2,000 kila mwaka nchini na wengine 60,000 kote ulimwenguni . Tatizo hili limezidi zaidi katika maeneo yaliyozongwa na umaskini kwa kuwa waathiriwa wengi hawana uwezo wa kutafuta tiba kwa dharura. Katika kampeini inayoendelea kwa sasa katika kaunti ya Laikipia, mbwa 1,500 wanatarajiwa kuchanjwa wakiwemo mbwa koko.