Walimu katika Kaunti ya Kilifi walazimika kutumia misitu kujisaidia
18th July, 2015
Hebu fikiria uwe mwalimu unayefundisha katika shule ambayo haina vyoo vya kujisaidia kwa zaidi ya miaka kumi. Kila unapotaka kwenda haja unakimbilia msitu ambao pia unatumiwa na wanafunzi wako. Mkimaliza mwarejea darasani kuendelea na masomo! Ndio uhalisia wa mambo yanayokumba baadhi ya shule katika eneo la magarini-kilifi.