Polisi wa Voi wakamata mwanamke kwa kosa ya kuuza bangi
17th July, 2015
Mwanamke mmoja mjini voi amekamatwa na maafisa wa polisi eneo hilo kwa kuuza bangi lakini alimsuta chifu aliyekuwa nao akisema kuwa pia chifu huyo anastahili kukamatwa kwani amekuwa akimruhusu kuendelea na biashara yake bora tu aendelee kuwa mpenzi wake. Mama beatrice manga ambaye ni mjane alisema kwa uchungu kuwa hana njia nyengine ya kuikimu familia yake na anaomba tu ajira mbadala badala ya kufungwa kwani hataki watoto wake wateseke.