Ubalozi wa Australia nchini Kenya umetoa msaada wa darasa la walemavu
9th July, 2015
Ubalozi wa Australia nchini Kenya umetoa msaada wa ujenzi wa darasa maalum la watoto walemavu katika shule ya msingi ya kangemi . Ubalozi huo umefanya hivyo ili kuwasaidia baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo ambao wanaishi na ulemavu. Shule hiyo ina jumla ya wanafunzi kumi na watatu wanaoishi na aina tofauti tofauti za ulemavu . Mbunge wa westlands tim wanyonyi alitoa wito kwa serikali kujenga madarasa ya aina hiyo kwa wanafunzi walemavu ili angalau wasihangaike sana wakiwa shuleni.