Jamaa adai vigogo serikalini wana njama ya kunyakua kipande chake cha ardhi Pipeline, Nairobi
7th July, 2015
Utata wa ardhi ya ekari 50 umejitokeza upya katika mtaa wa Pipeline, hapa jijini Nairobi baada ya mmiliki mmoja kudai kuwa wapo vigogo serikalini ambao wana njama ya kunyakua kipande chake cha ardhi licha ya yeye kuelekea mahakamani kusitisha ujenzi wa bomba la kupitisha majitaka kwenye aradhi yake.