Maafisa 28 kuondoka katika nyumba zinazomilikiwa na bandari ya Mombasa
5th July, 2015
Usimamizi wa bandari ya Mombasa sasa umewataka maafisa 28 walioachishwa kazi kwa kushiriki mgomo kuondoka mara moja katika nyumba zinazomilikiwa na bandari. Hatua ambayo imeshutumiwa vikali na chama cha wafanyakazi bandarini. Lakini jinsi mwanahabari wetu John Juma anavyoripoti kumeibuka mgawanyiko miongoni mwa wafanyakazi, wengine wakitaka chama chao kivunjiliwe mbali kwa kuongoza mgomo haramu.