ISIOLO ALLIENS: Wafungwa 80 raia wa Ethiopia wamesusia chakula katika Gereza la Isiolo
2nd July, 2015
Wafungwa 80 raia wa ethiopia wanaotumikia kifungo cha mwaka mmoja katika gereza la isiolo, wamesusia chakula kwa siku ya 3 mfululizo. Hii ni kwa sababu ya kupashwa habari kuwa familia zao nchini ethiopia zinahangaika huku baadhi wakifariki kutokana na matatizo wanayopata. Kama anavyoripoti ali manzu, wito umetolewa na kamanda wa magereza kaunti hiyo, kwa serikali kuwaachilia huru wafungwa hao.