Mwanafunzi atoweka baada ya kupachikwa miimba na mwalimu
29th June, 2015
Familia moja katika eneo la ruiyobei kaunti ya nakuru imekumbwa na hofu kufuatia kutoweka kwa binti yao, anayedaiwa kupachikwa mimba na mwalimu wake. Msichana huyo wa umri wa miaka 15 wa kidato cha pili, anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwalimu wake tangu akiwa darasa la nane, na hata alipoingia shule ya upili, mwalimu huyo aliendelea kumnyemelea kabla ya kumpa mimba hiyo. Kwa sasa msichana huyo ametoweka huku familia ikimtaja mwalimu wake kuwa mshukiwa mkuu.