Waziri Charity Ngilu afikishwa Mahakamani
26th June, 2015
Mapema leo waziri wa ardhi Charity Ngilu amepata pigo kwenye ombi lake la mapema wiki hii kwa mahakama kumwondoa kwenye kesi inayowajumuisha maafisa wengine wa wizara ya ardhi. Ngilu alitaka kesi inyomkumba kushughulikiwa tofauti lakini hakimu lawrence mugambi amedinda kufanya hivyo na kuagiza kwamba waziri huyo aliyesimamishwa kazi kwa muda atashirikishwa kwenye kesi ya ufisadi inayowakumba wadogo wake katika wizara ya ardhi.