Mahakama ya South Africa yamkataza Rais wa Sudan kutoka nchini humo
14th June, 2015
Mahakama moja nchini afrika kusini imetoa agizo la muda la kumzuia rais wa sudan omar al bashir kwa kutoka nchini afrika kusini .rais bashir alikuwa nchini humo akihudhuria kongamono la umoja wa afrika maarufu au. Mahakama ya kimataifa ya jinai, icc ilitoa agizo la kukamatwa kwa bashir mwaka wa 2009 , kwa tuhuma za mauaji yaliyoletwa na mapigano katika mji wa darfur kule sudan, hata hivyo rais bashir alipinga madai hayo. Baada ya agizo la kukamatwa kwake na icc, ziara za bashir zimekuwa katika mataifa yasiyokuwa chini ya mahakama hiyo kama vile, misri na saudi arabia. Marais hao walikuwa wamekutana mjini johannesburg, afrika kusini ili kuzungumza kuhusu swala tata linaloendelea kulikumba taifa la burundi , kongamano hilo linalongozwa na rais wa zimbabwe robert mugabe ambaye analipinga swala zima la mahakama ya ICC .