Shughuli za mafunzo katika Chuo cha KTTC yalikatizwa baada ya wanafunzi kugoma
11th May, 2015
Shughuli za mafunzo katika Chuo cha Kitaifa cha Mafunzo ya Teknolojia ya Elimu KTTC yalikatizwa baada ya wanafunzi kugoma wakimtaka mwalimu mkuu wa shule hiyo kuondolewa. Wanafunzi hao wanamlaumu mwalimu mkuu kwa kutowapa mabweni mazuri ya kulipia gharama hiyo kwenye karo ya shule. Wanafunzi hao wamesema kuwa wamelazimika kutafuta malazi mbadala nje ya shule. Wanadai pia kuna baadhi ya wanafunzi kama wanne hivi ambao wamefariki mwezi mmoja uliopita kutokana na ukosefu wa usalama.