Wakimbizi zaidi ya laki tatu kutoka Somalia wanaiomba serikali ya Kenya kutowafurusha toka Dadaab
9th May, 2015
Wakimbizi zaidi ya laki tatu kutoka nchini Somalia walioko katika kambi ya Dadaab wanaiomba serikali ya Kenya kutowafurusha kambini humo kutokana na hofu ya hali ya vita nchini kwao. Hata hivyo wasi wasi wao unajiri siku chache tu baada ya serikali kukubaliana na shirika la umoja wa mataifa la kushughulikia wakimbizi -UNHCR kwamba haitawalazimisha kurudi makwao.