Wauguzi wasitisha mgomo unaokuwa ukiendelea katika Kaunti ya Mombasa
20th April, 2015
Mgomo wa wauguzi katika kaunti ya mombasa umeingia siku ya tano bila suluhu yoyote kupatikana, hali ambayo imeacha maisha ya wagonjwa wengi hatarini. Mvutano sasa umeibuka huku kaunti ya mombasa ikifika mahakamani kuwalazimisha wauguzi kurejea kazini wakati ambao wauguzi hao kupitia katibu wao mkuu wanaihimiza serikali ya taifa kusimamia sekta ya afya wakidai serikali ya kaunti ya mombasa imelemewa na shughuli hiyo.