Mzee Daniel Moi ataka Rais Uhuru Kenyatta kuimarisha usalama nchini
4th April, 2015
Rais mstaafu daniel arap moi amekashifu vikali mauaji ya kigaidi yaliyotekelezwa katika chuo cha garissa na kusisitiza kuwa ni jukumu la serikali kuwahakikishia wakenya usalama wao. Mzee moi ameiomba serikali kutekeleza sera muhimu ili kutilia kikomo mauaji ya mara kwa mara humu nchini. Mzee moi pia ameitaka serikali kuwapa wakenya majibu kuhusu masuali muhimu yanayohusu usalama wa taifa.moi ametoa risala za rambi rambi kwa ndugu, jamaa na marafiki wa waliofariki. Rais mstaafu alikuwa akihutubu katika shule ya upili ya kapsabet wakati wa utoaji tuzo kwa wanafunzi waliofanya vyema kwenye mtihani wa kcse wa mwaka jana.