Waziri Ngilu hajafurahishwa na hatua ya Rais Uhuru Kenyatta ya kumtaka ajiondoe afisini
30th March, 2015
Waziri wa Ardhi Charity Ngilu amejiondoa afisini ili kutoa nafasi ya uchunguzi dhidi yake kufuatia madai aliyolimbikiziwa ya kuhusika kwenye ufisadi. Ngilu ambaye amekua waziri wa 5 kujiondoa mamlakani amewalaumu watu wenye ushawishi mkuu serikalini kwa masaibu anayoyapitia, huku akitoa hakikisho kwamba atarejea katika afisi zake zilizopo katika jumba la ardhi. Waziri Ngilu hajafurahishwa na hatua iliyochukuliwa na Rais Uhuru Kenyatta ya kumtaka ajiondowe,ingawa alikariri kuwa anaunga mkono vita dhidi ya ufisadi.