Mamia ya wakulima waandamana nje ya mabohari ya NCPB
18th March, 2015
Mamia ya wakulima wameegesha malori ya kubebea mazao yao na kuandamana nje ya mabohari ya bodi ya kitaifa ya nafaka na mazao NCPB, baada ya kuarifiwa kuwa serikali haitonunua mazao ya nafaka walioyatoa mashambani. Ilikua vigumu kwa maafisa wa halmashauri hio kuingia kazini hali iliotatizwa na magari yao kuifunga njia ya kuelekea lango kuu la afisi za bodi hio.