Shughuli ya uchujaji wa polisi sasa yaelekea kaunti ya Nakuru
3rd March, 2015
Uchujaji wa polisi sasa unaelekea kaunti ya Nakuru ambapo wanachama wa kamati ya uchujaji wakiongozwa na mwenyekiti wa tume ya huduma za polisi Johnstone Kavuludi kesho wataanza shughuli mjini nakuru.
Shughuli hiyo itawashirikisha maafisa 120 wenye ngazi za usimamizi kutoka kaunti za eneo la South Rft. Polisi hao wanaojumuisha wakuu wa polisi wilayani na katika kaunti wanatarajiwa kufika mbele ya kamati ya uchujaji kwenye utaratbu utakaochukua wiki moja. Shughuli hiyo itaelekea eneo la North Rift katika muda wa wiki mbili zijazo