Rais wa Namibia anayeondoka atuzwa tuzo ya Mo Ibrahim
2nd March, 2015
Rais wa Namibia anayeondoka Hifikepunye Pohamba ametuzwa tuzo ya Mo Ibrahim ya mwaka wa 2014 yenye thamani ya takriban milioni 450. Pohamba ametuzwa kwa kuwa kiongozi aliyezingatia demokrasia na kuboresha uchumi wa taifa la Namibia. Pohamba ametajwa kuwa kiongozi mwenye maadili na sera nzuri za uongozi.tuzo hiyo pia iliwavutia marais wengine wa Afrika akiwemo Rais mstaafu Mwai Kibaki pamoja na Armando Guebuzza wa msumbiji ambao pia walitazamiwa kuibuka washindi.