Wenyeji wa Kinangop wadai kutohusishwa vilivyo katika mpango wa kawi
27th February, 2015
Waziri wa kawi davies chirchir amesema kuwa serikali inafanya kila iwezalo kuona kwamba mahitaji ya wenyeji wa kinangop yameangaziwa. Wakaazi wa sehemu ya kinangop waliandamana hapa jijini wiki moja iliyopita wakimtaka rais kenyatta kuingilia suala hilo. Tangu kuanzishwa kwa mipango ya kuzalisha nguvu za umeme kutokana na upepo, visa vya uhalifu vimeongezeka wakati wakaazi hao wakijaribu kulinda ardhi yao.