Viongozi watoa hisia kali kutokana na uamuzi wa korti kusimamisha CDF
21st February, 2015
Wabunge wote 290 nchini walipata pigo jana baa da ya majaji wa mahakama kuu isaac lenaola, mumbi ngugi na david majanja kutoa uamuzi wa kufutiliwa mbali kwa uwepo wa pesa za ustawi wa maeneo bunge yaani cdf wakisema sheria ya mwaka wa 2013 iliyoidhinisha fedha hizo si halali. Tayari wabunge na maseneta wamepinga uamuzi huo ambao magavana na wakilishi wa wadi nchini wanaonekana kuufurahia ikizingatiwa kwamba sasa hao ndio watakao simmamia pesa zote za maendeleo mashinani. Kwenye hesabu ya mwaka wa 2014/2015 cdf ilitengewa bilioni 31.5 tofauti na bilioni 22 za mwaka uliotangulia.baadhii ya wabunge wameapa kuupinga uamuzi huo bungeni.