Wakenya walaumu serikali kwa kuzima masafa ya vyombo vya habari
21st February, 2015
Wakenya hawajaridhika na njia mpya za kupata habari baada ya kufungwa kwa masafa ya kupeperushia habari ya stesheni nne za KTN, Citizen, NTV na QTV. Wakenya wameitwika serikalilawama za kuzima masafa hayo. Aidha, tofauti na madai ya mamlaka ya mawasiliano kwamba vidubwasha vilivyo nchini vinatosha, wakenya wengi wamekiri kuwa hawana.