Aliyekuwa dereva wa marehemu George Muchai azikwa
18th February, 2015
Jamaa na marafiki wa aliyekuwa dereva wa marehemu George Muchai ambaye pia aliuawa wakati mmoja na mwajiri wake, wamejumuika nyumbani kwake katika eneo la Mukurweini kwa hafla ya mazishi. Kamanda wa polisi katika kaunti ya Nairobi Benson Kibue amewakilisha idara ya polisi ambapo ametoa onyo kwa wanaohusika kwenye uhalifu na mauaji ya kiholela.