Zaidi ya washirika 15000 kushiriki makala ya pili ya mashindano ya mbio za First Lady
12th February, 2015
Makala ya pili ya mashindano ya mbio za first lady ambayo yatafanyika tarehe 8 mwezi huu yatamalizika katika uwanja wa Nyayo huku washiriki zaidi ya 15000 wakitarajiwa kushiriki. Makala ya kwanza ya mbio hizi yalioanzishwa mwaka uliopita na mke wa rais wa kenya, Bi Margaret Kenyatta yalimalizika katika eneo la Uhuru gardens kwenye barabara ya Langata. Washiriki 12000 walijitokeza mwaka uliopita. Huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka mwaka huu, waandalizi wa mashindano haya wamedokeza kuwa watakaomaliza katika nafasi ishirini za kwanza watatuzwa huku mshindi wa kilomita 21 akipata 750,000, mshindi wa mbio za kilomita 10 atapata kitita cha shilingi 250,00.