Serikali yaanza kuwasajili kuwa raia watu ambao wameishi humu nchini kwa miaka mingi
12th February, 2015
Serikali imeanza kuwasajili kuwa raia watu wa mataifa mengine ambao wameishi humu nchini kwa miaka mingi. Hatua hiyo itahakikisha watu hao wamepata vitambulisho vya taifa. Shughuli hiyo imeanzia kaunti ya Kwale ambako jamii ya Wamakonde kutoka msumbiji imekuwa ikiishi kwa zaidi ya miaka 50.