Sam Shollei asema Standard Group itashirikiana na serikali za kaunti kuhakikisha ugatuzi unafanikiwa
29th January, 2015
Mfumo wa ugatuzi ndio bora zaidi kwa wakenya hasa kwa kuwa umepeleka huduma za serikali mashinani. Kwenye kikao na gavana wa Nandi Dakt Cleophas Lagat, afisa mkuu mtendaji wa Standard Group Sam Shollei amesema kutokana na hayo shirika hili la habari litashirikiana na serikali za kaunti kuhakikisha kwamba mfumo huo unafanikiwa. Kwa upande wake Gavana Lagat ameelezea furaha kwa mchango wa vyombo vya habari kwenye oparesheni za serikali za kaunti