Wanafunzi wa vyuo vikuu kupokea fedha za mkopo wa HELB
26th January, 2015
Wanafunzi wa vyuo vikuu wana kila sababu ya kusherehekea baada ya fedha za mkopo wa HELB kutolewa. Serikali ikiwa imetoa shilingi bilioni 1.4 kati ya bilioni 6.8 zilizotarajiwa. Takriban wanafunzi elfu 65 walijisajili kupokea mikopo hiyo baada ya kutaka kufanya mgomo kutokana na kuchelewa kutolewa kwa fedha hizo. kulingana na maafisa wa HELB ni kwamba kumekuwa na ongezeko kuu la wanafunzi wanaojisajili kupokea mikopo hiyo. Wanafunzi hii leo walionekana kufurika katika afisi za HELB wakituma maombi ya mikopo ndiposa waendelee na masomo yao ya vyuo vikuu.