Wanafunzi wa Lang'ata watupiwa vitoa machozi kwenye mzozo wa ardhi
19th January, 2015
Maandamano katika shule ya msingi ya barabara ya langata yalibadilika kuwa vioja pale maafisa wa polisi walipowatawanya wanafunzi kwa kutumia vitoa machozi. Wanafunzi watano wa shule hiyo walipelekwa hospitali kutibiwa, huku afisa mmoja wa polisi akijeruhiwa. Na kama anavyoarifu mwanahabari Mohamed Mahmoud, hatua ya maafisa wa polisi ya kuwarushia wanafunzi vitoa machozi imezua mijadala mbali mbali miongoni mwa wakenya.