Mzozo wa ardhi ya shule ya msingi ya Lang'ata yaibuka
16th January, 2015
Mzozo wa umiliki wa kipande cha ardhi ya kiwanja cha kuchezea mpira cha shule ya msingi ya Lang’ata umechukua mwelekeo mpya baada ya aliyekuwa meya wa baraza la jiji la nairobi Geoffrey Majiwa pamoja na mbuge wa makadara benson mutura kudaiwa kujitokeza na kudai kuwa ni wamiliki wa kampuni ya airport view housing inayomiliki kipande hicho cha ardhi. Ikifanya ziara katika ardhi hiyo, tume ya ardhi imegundua kuwepo kwa hati miliki aina mbili za ardhi hio.