Jamaa aponea kifo baada ya tinga tinga kuangukiwa na jumba lililokuwa likibomolewa
15th January, 2015
Jamaa mmoja ameponea kifo katika mtaa wa Kasarani hii leo alipokuwa akibomoa jumba moja lililotangazwa na usimamizi wa kaunti ya nairobi kuwa lilikuwa hatari mno kutumika kama sehemu ya kuishi.jumba hilo lenye ghorofa nne liliporomoka na kumuangukia wakati jamaa huyo alipokuwa akilibomoa kwa tingatinga . Jamaa huyo alijitoa kwenye kifusi kilichokuwa kimejaa vumbi na kuchukuliwa na maafisa wa kaunti waliopmpeleka kwa matibabu. Wapangaji wa jumba hilo walihama disemba mwaka jana baada ya kuagizwa na mwenye jumba kuondoka ili lifanyiwe marekebisho. Hata hivyo, jumba hilo lilionekana kuanza kuzama wakati huo na kuwalazimisha maafisa wa kaunti kuchukua hatua ya kulibomoa.