Maelfu ya watu wahudhuria mazishi ya Fidel Odinga
10th January, 2015
Marehemu fidel castro odinga amezikwa katika shamba la babu yake jaramogi oginga odinga kang'o kajaramogi eneo la bondo, kaunti ya siaya. Zaidi ya waombolezaji 10,000 wamejimuika na familia ya raila odinga katika uwanja wa chuo kikuu cha bondo, kwa ibada ya wafu kwa ajili ya marehemu mazishi ya fidel. Familia ya marehemu fidel imemtaja kuwa mtu aliyependa kuunganisha na kujumuika na watu. Dadake fidel, rosemary odinga amesema kifo cha fidel ni mwaliko kwa wakenya na hasa wanasaisa kushirikiana katika kutatua masuala ya taifa hili. Na jamii zingine na kuwataka wakenya kuiga mfano huo na kutangamana bila kujali kabila zao. Aidha raila odinga amesema amepoteza rafiki wa dhati na mtu mnyenyekezu na aliyejitolea kusaidia jamii huku mkewe ida odinga akisema fidel alikuwa mtoto mwenye tabia ya kipekee. Miongno mwa waliofika kuomboleza na familia ya odinga, ni aliyekuwa waziri mkuu wa zimbabwe morgan tsvangirai, mwakilishi wa rais yoweri museveni viongozi wengine kutoka afrika mashariki na v