Amir Khan azuru na kutoa msaada kwa Wapaskistani
27th December, 2014
Mwanamasumbwi amir khan wa uingereza amedokeza atapeana kaptula ya zaidi ya pauni 30,000 za uingereza ili kusaidia kuikarabati shule iliyoshambuliwa na kundi la taliban na kupelekea vifo vya watu 141. Khan, amabaye ana asili ya ki-pakistan alivaa kaptula hiyo yenye mkanda wa dhahabu pale alipotetea taji lake la wbc uzani wa welter dhidi ya devon alexander jijini las vegas marekani. Khan mwenye umri wa miaka 28 alisema kuwa alipata msukumo wa kutoa msaada baada ya kuzaliwa kwa mwanawe. Msaada wake unanuia kuikarabati shule ya peshawar, ambako wanafunzi 132 waliuawa wakati wa shambulizi la taliban mapema mwezi huu.