Shirika la Reli ya RVR yaagiza mabogi zaidi nchini
27th December, 2014
Shirika la reli la Rift valley railways linapania kuongeza idadi ya shehena zake inazozisafirisha kati ya mombasa na taifa jirani la uganda ifikapo mwaka ujao. Hatua hii inajiri baada ya kuwasili kwa mabogi mengine mapya katika bandari ya mombasa mapema hii leo. Akizungumza wakati wa kuyapokea mabogi hayo ya gari moshi mhandisi mkuu wa rvr Oliver Omondi alisema kuwa usafirishaji wa shehena katika sehemu nyengine za nchi utaimarika pakubwa hasa ikizingatiwa kuwa matumizi ya reli yalipuuzwa kwa muda mrefu na badala yake wengi wa wasafirishaji wakaamua kutumia matrela katika kusafirish mali zao. Mabogi matatu ndio yaliyowasili hii leo ikiwa ni kati ya shehena ya mabogi ishirini yaliyonunuliwa na rvr kwa thamani ya billioni mbili nukta mbili.