Washukiwa kumi wa ugaidi wafikishwa mahakamani
22nd December, 2014
Washukiwa 10 wa ugaidi wanaoaminika kumuua afisa wa usalama mnamo tarehe 11 mwezi huu katika eneo la kaloleni kaunti ya kilifi ,walifikishwa katika mahakama ya mombasa asubuhi ya leo. Washukiwa hao ambao walifikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali walipatikana na hatia ya wizi wa kimabavu. Hatahivyo walikana madai hayo mbele ya jaji wa mahakama ya mombasa. Licha ya mwendeshaji mashataka kutaka 10 hao wasiachiliwe kwa dhamana, hakimu mtendaji wa mahakama ya mombasa alisema kesi hiyo itaskizwa januari mwaka ujao ili kutoa hukumu ya kesi hiyo.