Vurugu na zogo kutokea bungeni baada ya upande wa serikali kuupitisha mswada wa sheria za usalama
18th December, 2014
Upande wa serikali bungeni umetumia wingi wake kuupitisha mswada wa sheria za usalama katika mazingira ya vurugu na zogo ambapo spika Justin Muturi amezingirwa na walinzi wa bunge. Aidha, imekuwa siku ambayo wakenya wameshuhudia mienendo ya fedheha miongoni mwa wabunge katika kikao mahsusi kilichoitishwa kukamilisha mswada huo. Upande wa upinzani ulianza mapema kutatiza utaratibu wa mjadala katika hatua iliyobadilisha bunge kuwa jumba la sarakasi