Raila Odinga apasha misuli moto ili kuingia katika bunge kwa kuwania kiti cha useneta,
7th December, 2014
Hatimaye sasa imeibuka kwamba kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga anapasha misuli moto ili kuingia katika bunge kwa kuwania kiti cha useneta, kaunti ya Homa-Bay. Frank Otieno alihudhuria kikao maalum nyumbani kwake Raila huko Bondo, ambapo ishara zipo kwamba mipango inaendelea kukamilika kumpokeza Raila kiti hicho kilichowachwa wazi baada ya kifo cha Seneta Otieno Kajwang’. Je , Raila akikubali uamuzi huu utakuwa ni mwanzo wake wa kujimaliza kisiasia au kujiimarisha Zaidi