Vyama mbali mbali na viongozi watoa hisia zao kuhusiana na Mauaji ya timbo la Mawe mandera
3rd December, 2014
Kufuatia ongezeko la ukosefu wa usalama nchini huku kisa cha hivi karibuni kikiwa shambulizi la Mandera mapema hii leo ambapo watu 36 waliuawa katika Mgodi, vyama mbali mbali vikiwemo muungano wa madaktari nchini, muungano wa wanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi SONU mashirika ya kijamii na chama cha CORD pamoja Na Gavana wa Mandera Aili Roba vimetoa hisia zao za kutoridhishwa na utovu huu wa usalama na kutaka serikali kuwajibika zaidi.