Tuzo za mwanaspoti bora za Soya zimepata udhamini kutoka kampuni ya Safaricom
27th November, 2014
Tuzo za kila mwaka za mwanaspoti bora za soya zimepata udhamini wa slihingi milioni kumi na mbili kutoka kwa kampuni ya mawasiliano ya safaricom. Kinyume na ilivyokuwa mashindano hayo kuandaliwa desemba kila mwaka, msimu huu waandalizi waliamua kusongeza tuzo hizo hadi januari tarehe 16 mwaka ujao. Mwenykiti wa tuzo hizo za soya evelyn watta alidokeza kuwa walifanya hivyo ili kuwapa fursa wanaspoti wanaoshiriki michezo kama vile magongo na mpira vikapu kwani wao hukamilisha ligi yao mwezi Desemba.