Joseph Kiplimo na Alice Aprot Beat ndio washindi wa makala ya 4 ya mbio nyika za Tuskeys Wareng
23rd November, 2014
Bingwa wa nishani ya fedha wa bara Afrika katika mita elfu tano Joseph Kiplimo na bingwa wa zamani wa mbio za nyika za barani Alice Aprot Beat ndio washindi wa makala ya nane ya mbio nyika za Tuskeys Wareng. Aidha kivutio katika mbio hizo mapema hii leo ni bingwa mara mbili wa dunia Vivian Cheruiyot aliyemaliza wa nne hiyo ni baada ya kurejea kwenye riadha baada ya miaka miwili.