Wakaazi wa Makueni waomba Rais Kenyatta kuivunjilia mbali serikali ya Kaunti hiyo
21st November, 2014
Wakaazi wa Kaunti ya Makueni wamefuganya virago na kuja hapa Nairobi ili kuwasilisha ombi kwa Rais Kenyatta kuivunjilia mbali serikali ya Kaunti hiyo. Wakazi hao wanadai kuwa wawakilishi wa wodi ni walafi na wameshindwa kujenga Kaunti. Haya yanaripotiwa huku mustakabali wa gavana Kivutha kibwana ukiwa mbele ya Mahakama na Seneti kufuatia hatua ya wawakilishi wa wadi kupitisha hoja ya kutokuwa na imani naye. Francis Mtalaki na taarifa hiyo.