Ndovu ni adui mkubwa Taita Taveta kwa uvamizi na uharibifu unaowafanya wakaazi kusalia fukara
16th November, 2014
Kwa wengi ndovu ni baadhi ya wanyama ambao ni kitega uchumi katika sekta ya utalii lakini kwa baadhi ya wakaazi Kaunti ya Taita Taveta mnyama huyu ni adui mkubwa kutokana na kuvamiwa na ndovu na uharibifu ambao wamedai kuwafanya wao kusalia fukara. Francis Mtalaki alizuru kaunti ya Taita Taveta na kutuandalia masaibu wanayopitia wakaazi wanaoishi katika mpaka wao na mbuga ya wanyama pori ya Tsavo.